Tuesday, June 23, 2015

Msiba Houston, Texas

Marehemu Edmund Mushi enzi za uhai wake
Wanajumuiya,

Kwa masikitiko makubwa, tunasikitika kutangaza kifo cha mwanajumuiya mwenzetu 
Bw. Edmund Mushi.

Ndugu yetu Edmund amefikwa na mauti usiku wa kuamkia leo June 23, 2015 katika hospital ya Houston Northwest Medical Center alipokuwa amelazwa.

Tunatoa wito kwa wanajumuiya kuwa na subira katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo. Taarifa zaidi za hatua itakayofuata zitatolewa mara tu baada ya kumalizika kwa kikao cha wanandugu wa karibu baadaye mchana huu.

Kwa niaba ya Jumuiya, tunatoa pole kwa ndugu, jamaa, na marafiki wa marehemu.

Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi

Asanteni,

Arnold Maira,
THC-Interim Spokesman.

No comments:

Post a Comment