Monday, April 24, 2017

WANAJUMUIYA WA HOUSTON WAFANYA KUMBUKUMBU YA MWAKA MMOJA WA KIFO CHA ANDREW NICKY SANGA

Jumuiya ya Watanzania waishio katika jiji la Houston , Texas  siku ya Jumamosi tarehe 04/22/2017 walifanya kumbukumbu ya kutimia kwa mwaka mmoja tokea mwanajumuiya mwenzao Bw. Andrew Nicky Sanga alipofariki dunia. Shughuli hiyo iliyohudhuriwa na watanzania wengi kutoka jimbo la Texas na majimbo mengine ya hapa Marekani ilianza kwa ibada fupi iliyoongozwa na Rev. Godwin Chilewa iliyofanyika kwenye eneo ambalo marehemu Andrew alipata ajali.

Baada ya ibada wanajumuiya walikutana kwa chakula cha usiku na vinywaji katika ukumbi wa 7 Star Cafe uliopo 14144 Westheimer Rd. Houston Texas 77077

Pata picha za tukio hilo hapa chini :

Mama mtoto wa marehemu Andrew, Emmy akiwa na bint wao Zoe

Wanajumuiya wakiwa katika ibada

Marafiki wa karibu wa marehemu Andrew kushoto ni Deo Temba na Wash Drew

Dr. Jenga, John na Re. Chilewa
Rais wa Jumuiya ya Watanzania Bw. Daudi Mayocha akizungumza


















































































































































































No comments:

Post a Comment